Juzi, Eva ambaye anasoma Shule ya Sekondari Mlowa mkoani
Iringa, alimkabidhi barua nyingine ya kampeni yake ya kupambana na uhaba wa
maji, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aliyoianzisha kutokana na majibu
aliyoandikiwa na Rais Obama akieleza matatizo yaliyopo katika Jimbo la Isimani
mkoani humo.
Mwanafunzi wa kidato cha pili, Eva Shedrack (16) ameanzisha kampeni
ya kupambana na uhaba wa maji baada ya kupokea majibu ya barua yake
aliyoandikiwa na Rais Barack Obama wa Marekani.
Awali, Eva alimwandikia barua rais
huyo akieleza kuhusu uhaba wa maji nchini ambayo ilisomwa katika baraza
kuu la Umoja wa Mataifa (UN), Septemba mwaka jana.
Juzi, Eva ambaye anasoma Shule
ya Sekondari Mlowa mkoani Iringa, alimkabidhi barua nyingine ya kampeni yake ya
kupambana na uhaba wa maji, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aliyoianzisha kutokana
na majibu aliyoandikiwa na Rais Obama akieleza matatizo yaliyopo katika Jimbo
la Isimani mkoani humo.
Katika barua yake kwa Waziri Mkuu,
Eva alisema ameanzisha kampeni hiyo inayojulikana kwa jina la ‘Simama na Eva’
ambayo imejipanga kusaidia kutatua kero ya maji vijijini.
No comments:
Post a Comment