Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda akimpongeza Mkurugenzi wa WCB, msanii Naseeb Abdul 'Diamond Platinumz' mara baada ya kumtembelea ofisini kwake na kutoa mchango wake wa madawati yapatayo 600 kwa ajili ya kuchangia maendelea ya mkoa. Akiongea katika makabidhiano hayo msanii huyo alisema ni jambo jema kwao kuweza kujitolea mchango huo ili kuweza kumuunga mkono Mhe. Makonda katika kukabilana na changamoto za elimu.
Mkurugenzi wa WCB, msanii Naseeb Abdul 'Diamond Platinumz' akiongea mara baada ya kukabidhi msaada wa madawati yapatayo 600 kwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaa.
Makonda akitoa shukrani zake za pekee kwa Mkurugenzi
wa WCB, msanii Naseeb Abdul 'Diamond Platinumz' kwa kuweza kutoa madawati 600
ikiwa ni mchango wake katika elimu ya kuweza kufanya wanafunzi kukaa sehemu
salama. Mhe. Makonda alisema kuwa wakati umefika kwa wasanii wakaweza kujitoa
katika jamii ambayo imekuwa ikiwapa wao sapoti na msanii Diamond amekuwa wa
kwanza
kuonyesha moyo wa pekee kwa kurudisha fadhila.
Makonda akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa WCB
mara baada ya kumtembelea ofisini kwake.
No comments:
Post a Comment